Gavana Joho ni 'Slay King' na sioni tatizo hata kidogo - Esther Passaris

- Esther Passaris alisema hakuna tatizo kwa mtu yeyote kujishaua ila wengi wamekosa kuelewa dhana yake - Kulingana na Passaris kujishaua ni kujipenda kwa vyovyote vile na kuelewa unachotaka maishani - Passaris alidai kuwa gavana Joho ni mfano bora wa 'Slay King' kwa sababu ya picha za kupendeza ambazo yeye hupakia kwenye mitandao akiwa amevalia

- Esther Passaris alisema hakuna tatizo kwa mtu yeyote kujishaua ila wengi wamekosa kuelewa dhana yake

- Kulingana na Passaris kujishaua ni kujipenda kwa vyovyote vile na kuelewa unachotaka maishani

- Passaris alidai kuwa gavana Joho ni mfano bora wa 'Slay King' kwa sababu ya picha za kupendeza ambazo yeye hupakia kwenye mitandao akiwa amevalia mitindo kadhaa ya kimavazi

Mwakilishi wa wanawake kaunti ya Nairobi Esther Passari amedai kuwa ni vema mtu kuwa Slay Queen au Slay King kulingana na jinsi anavyotaka mwenyewe.

Habari Nyingine : Binti mrembo ashangaza wengi baada ya kutangaza anaishi na virusi vya HIV

Habari Nyingine : Gavana adaiwa kupofuka, hajaonekana kwa kipindi cha miezi 6

Kulingana na Passaris watu wengi wamekosa kuelewa dhana ya kujishaua ila yeye haoni tatizo lolote mtu kujipenda, ajipodoe, apigwe busu, apige picha na kisha aichapishe mitandaoni.

Akizungumza na runinga ya Ebru, Passaris aliwaelezea Wakenya maana ya kuwa slay queen au slay king huku akidai kuwa gavana wa Mombasa Hassan Joho ni mfano bora Slay King.

Habari Nyingine : Dereva wa tuktuk anaswa kwenye video akiwatwanga polisi trafiki

Passaris alisema gavana Joho huvutia sana kwenye picha zake hasa kulingana na jinsi yeye huvalia mavazi ya miundo ya kipekee.

" Kujishaua ni kujipenda tu kwa ujumla, kujipaka rangi ya mdomo (lipstick), kupigwa busu na kisha kupigwa picha. Hii sio ukahaba kama wengi wanavyodhania, ningependa wasichana wote wajishaue jinsi wapendavyo, hata mimi mwenyewe nimewahi kujishaua na mwanangu kwenye picha," Passaris alisema.

Habari Nyingine : Mtangazaji Mary Kilobi adhibitisha yeye ni mke nambari 3 wa Atwoli

" Unapomuona gavana Joho akichapisha mitandaoni picha zake akiwa anapendeza na hakuna mtu wa kumsuta, hiyo ndiyo 'kuslay' hasa wafuasi zaidi ya 4000 wakitoa maoni ya kupendezwa na picha yake," Passaris aliongezea.

READ ENGLISH VERSION

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke ,kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Tazama habari zaidi kutoka TUKO TV

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdibn91hZJmnpqukaOubrbOoaZmppliwK2t2GaioqaXYruiedKipqehXamutbXZqGShmaSWeqy1w6ieqGWVqMGpsdFmp5qro5a%2Fqr%2BNoaumpA%3D%3D

 Share!