Mvua kubwa yatatiza shughuli Nairobi kwa mafuriko (picha)

- Mvua kubwa inayoendelea kunyesha imesababisha mafuriko katika barabara nyingi jijini Nairobi na kuwatatiza watu wanaotembea kwa miguu na madereva wa magari kuyatumia - Mvua hiyo iliyonyesha Alhamisi, Machi 15 asubuhi ilisababisha misongamano mikubwa ya magari huku wakazi wa jiji wakijaribu kupita kwenye maji na matope

- Mvua kubwa inayoendelea kunyesha imesababisha mafuriko katika barabara nyingi jijini Nairobi na kuwatatiza watu wanaotembea kwa miguu na madereva wa magari kuyatumia

- Mvua hiyo iliyonyesha Alhamisi, Machi 15 asubuhi ilisababisha misongamano mikubwa ya magari huku wakazi wa jiji wakijaribu kupita kwenye maji na matope

- Sehemu ya barabara ya Nairobi-Narok eneo la Mai Mahiu iliharibiwa na mvua kusababisha shimo hubwa, hali iliyokatiza shughuli za usafiri katika barabara hiyo

- Idara ya utabiri wa hali ya anga ilitoa onyo kuwa kungeshuhudiwa mvua kubwa na mafuriko

Barabara nyingi jijini Nairobi siku ya Alhamisi, Machi 15 asubuhi ziligeuka mito kutokana na mvua kubwa iliyonyesha.

TUKO.co.ke imedhibitisha kuwa baadhi ya barabara zenye shughuli nyingi jijini zilifurika na kuwatatiza wanaotembea kwa miguu na madereva kuyatumia.

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Habari Nyingine: Idara ya hali ya anga yatoa orodha ya maeneo 25 yatakayoathiriwa na mafuriko, Nairobi

Habari Nyingine: Polisi wa kike ashtakiwa kwa kuchasha picha za ‘utupu’ mtandaoni

Mvua hiyo ilisababisha misongamano mikubwa ya magari huku wakazi wa jiji la Nairobi waliokuwa wakielekea kazini waking’ang’ana kupita kwenye maji hayo.

Maeneo yaliyoathirika ni barabara za Forest, Uhuru, Juja-Pangani, Bangladesh-Rongai na mzunguko wa Globe.

Hizi ni picha zinazoonyesha hali ilivyokuwa:

Siku moja iliyopita sehemu katika barabara ya Nairobi-Narok katika eneo la Mai Mahiu ilizama na kusababisha msongamano wa magari huku wasafiri wengine wakilazimika kutumia barabara zingine.

Habari Nyingine: Jamaa ajuta baada ya kupatikana 'akichota maji katika kisima cha wenyewe'

Idara ya utabiri wa hali ya hewa ilionya kuwa kungekuwa na mvua kubwa na mafuriko katika maeneo ambako mafuriko hushuhudiwa.

Idara hiyo ilisema kuwa maeneo ya Nairobi, magaribi, mashariki, kati mwa kenya na katikati ya bonde la ufa yangeshuhudiwa mvua hiyo kubwa.

Habari Nyingine: Mambo 7 yaliyomo kwenye makubaliano mapya kati ya Uhuru na Raila

Mamlaka ya kukarabati barabara kuu nchini (KeNHA) Alhamisi, Machi 15 iliwatahadharisha wanaotumia barabara zote kuwa waangalifu wakati wa msimu wa mvua.

“Tunawaomba wasafiri wote kuwa waangalifu wakati wa msimu wa mvua. KeNHA itaendelea kuwapa habari za sehemu zozote za barabara zitakazoathirika.” Taarifa ya KeNHA ilisema.

Read ENGLISH VERSION

Una taarifa moto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke , kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma wagoma | TUKO TV

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2Bvzmeinmdia4V4fJRmpK%2BtkWK4tq7WmmSymaSWwarGwGaqoa2XncKttYynmKKqn5e2brfWmmSmmZaqv6q3zmanopuYlnupwMyl

 Share!