Sababu ya Jomo Kenyatta kumtaka Nkaissery kufika kwake

-Kazi ya marehemu Joseph Nkaissey kama mwanajeshi ilianzia kwa changamoto kubwa - Alikuwa miongoni mwa waliobahatika kupokea mafunzo nchini India -Baada ya kurudi nchini, alikataa kurudi katika chuo cha mafunzo ya kijeshi na kukaidi wakubwa wake

-Kazi ya marehemu Joseph Nkaissey kama mwanajeshi ilianzia kwa changamoto kubwa

- Alikuwa miongoni mwa waliobahatika kupokea mafunzo nchini India

-Baada ya kurudi nchini, alikataa kurudi katika chuo cha mafunzo ya kijeshi na kukaidi wakubwa wake

- Alikuwa Mkenya wa kwanza kuitwa mbele ya Mzee Jomo Kenyatta kwa kukaidi amri hiyo

Marehemu Meja Jenerali Joseph Nkaissery anaendelea kupongezwa kwa uwezo wake na msimamo wake mkali katika uongozi baada ya kuaga dunia ghafla Jumamosi Julai 8.

Habari Nyingine: Picha ya mtangazaji maarufu wa runinga akiwa katika shule ya upili itakuvunja mbavu

Katika mahojiano ya awali na K24 Desemba 26, 2014, alibainika kama mtu mwenye furaha na mcheshi alipokuwa akizungumzia jinsi alivyojiunga na jeshi.

Alieleza kuwa kwa wakati mmoja aliitwa na Hayati Mzee Jomo Kenyatta, “Niliingia jeshi kutoka chuo kikuu. Nilipewa mafunzo katika taasisi ya mafunzo ya kijeshi Lanet kwa miezi minne kabla ya kuhamishiwa shule nyingine ya kijeshi.

Pakua APP mpya ya TUKO upate habari BURE!

Mwaka wa 1973, alikuwa miongoni mwa waliofaidika kwenda mafunzo ya kijeshi India.

Mara ya mwisho kuonekana kwa umma ilikuwa wakati wa mkutano wa maombi Uhuru Park Ijumaa Julai 7.

Habari Nyingine: Zaida ya wanasiasa 10 wa Jubilee wahamia NASA

Lakini mafunzo yake India pia yalikabiliwa na matatizo kwani baada ya Idi Amin kufukuza Wahindi Uganda, Waafrika walianza kulengwa India, hivyo akarudi nchini miezi mitatu kabla ya kuhitimu.

Kwa sababu hakuhitimu, aliamua kurudi katika Chuo Kikuu cha Kenyatta hata ya kutakiwa na makamanda wake kurejea tena kwa mafunzo ya kijeshi.

Alikataa kwa sababu mafunzo ya kijeshi na magumu sana. Katika mafunzo hayo, alikuwa na mpwawe Kenyatta, Kungu.

“Tulikamatwa na kupelekwa mbele ya Mzee. Ni mimi Mkenya wa kwanza kupelekwa mbele ya rais kwa kukataa agizo,” alieleza.

Rais alimwambia ilikuwa lazima kwake kufuata maagizo au aende katika jela la Kamiti. Walikataa, na ikambidi Mzee kupanga mafunzo maalum kwao.

Habari Nyingine: Nani ataweza kunyakua urais kati ya Uhuru na Raila? Pata kujua kutoka kwa utafiti wa hivi punde

“Wakati wa kuhitimu, Rais alinitambua, akaniita na kuniambia kuwa nitakuwa kiongozi mkubwa,” Nkaissery alieleza.

Subscribe to watch new videos

Subscribe to Tuko youtube channel to watch more interesting videos

Read ENGLISH VERSION

Una maoni? Una habari ambayo ungependa tuichapishe?Tuma ujumbe kwa mhariri:mwangi.muraguri@tuko.co.ke

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiaYNxfpRmqpqakZfCbsXAZqGopZ9iuKa62JqrrZldoMKuwMCkmGamm5a2tL%2FEq7Bmo6WbtqytjKSumqOVY7W1ucs%3D

 Share!